Header Ads

ATLETICO MADRID YAING'ANG'ANIA REAL MADRID

Kikosi cha Real Madrid kimelazimishwa sare katika Uwanja wake wa nyumbani dhidi ya Atletico de Madrid kwa sare ya mabao 1-1.

Mabao ya mchezo huo yamefungwa katika dakika ya 53 kwa Real Madrid na dakika ya 57 kwa Atletico kupitia Antoine Griezmann.

Ronaldo amefikisha bao lake la 23 msimu huu kwenye La Liga huku akiachwa kwa mabao 6 dhidi ya mpinzani wake, Lionel Messi aliye na 29.

Real imeendelea kusalia kwenye nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kwa kuwa na alama 64 dhidi ya 68 za Atletico, wakati vinara FC. Barcelona wakiwa na pointi 79.

No comments