Header Ads

MWENGE WA UHURU KUWASHWA LEO

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Aprili 2,2018 atawasha Mwenge wa Uhuru mkoani Geita.

Sherehe za kuwashwa Mwenge zinatarajiwa kuanza saa moja asubuhi hadi saa tano asubuhi katika kiwanja cha Magogo mjini Geita.
Mwenge wa Uhuru ambao utakimbizwa mkoani Geita kwa siku sita  utakabidhiwa mkoani Kagera Aprili 7,2018.

Mbio za Mwenge ambazo kauli mbiu kwa mwaka huu ni ‘Elimu ni ufunguo wa maisha, wekeza sasa kwa maendeleo ya Taifa zitahitimishwa Oktoba 14,2018 mkoani Tanga.

No comments