Header Ads

RAIS JOHN POMBE MAGUFULI AMZUNGUMZIA MAKONDA

Dar es Salaam. Rais John Magufuli amezungumzia elimu ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa madai kwamba suala hilo lilianzishwa wakati kiongozi huyo alipojaribu kuwakamata wahusika wa dawa za kulevya.
Hata hivyo, alisisitiza kwamba elimu yake (Makonda) siyo kitu kwake na kwamba hata angekuwa hajui kusoma yeye ni bora kwake kwa sababu anafanya kazi nzuri ambayo hata baadhi ya waliosoma hawaifanyi.
Rais Magufuli aliyasema hayo leo Jumanne wakati akifungua mkutano mkuu wa 33 wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) uliofanyika jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa pia na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

No comments