Header Ads

Bodaboda yapigwa stop Zanzibar


Serikali imesema haijatoa lesseni za usafiri wa pikipiki (bodaboda) kusafirisha abiria kwa njia ya biashara  na atakae  tumia  bodaboda kusafirisha abiria atakuwa ametenda  kosa kisheria hivyo hatua kali zitachukuliwa.
Naibu Waziri wa Ujenzi,Mawasiliano na Usafirishaji Mohammed Ahmda Salum amesema licha ya kuwa serikali haina ajira za kutosha  lakini ajira ya bodaboda bado haijaruhusu kufanyika Zanzibar kutokana  na athari  nyingi zinazotokea  zinazotokana na  bodaboda hizo.
Amesema Serikali  inawashauri vijana  kufanya ajira  halali zilizoruhusiwa  kisheria  ili kuepusha mizozo na  serikali  na kutoa wito kwa waendesha pikipiki kuwa makini na kufuata sheria wanapokuwa barabarani ikiwemo kuvaa kofia ngumu  ambayo itamkinga  endapo watapata ajali.

No comments