Header Ads

DR.SHEIN KULIPA MADAI YA WAALIMU ZANZIBAR



Ikiwa serikali ya Tanzania bara ikikamilisha uamzi wa kulipa malimbikizo ya wafanyakazi na watumishi wa umma wakiwemo na waalimu.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi Zanzibar Dr. Ali Mohammed Shein amesema sera ya elimu bure  kwa wanafunzi wa sekondari itaanza ifikapo  mwezi june  mwaka huu.
Amesema hayo wakati akizungumza  katika Mkutano Mkuu wa Sita wa chama cha walimu Zanzibar  amesema serikali imeamua  kuondoa ada  kwa wanafunzi  kwa lengo la kuendeleza sera ya rais wa awamu ya kwanza Shekh Abeid Amani Karume.
Amesema  sera ya elimu bure itaimarika endapo walimu watafanya kazi kwa mujibu wa sheria na maendeleo ya elimu yatajengeka iwapo  walimu watakuwa na juhudi  na uimara pamoja na misingi  bora na zamira njema ya kufundisha wanafunzi mashuleni.
Dr. shein amesema anatambua matatizo yanayowakabili walimu   yakiwemo uhaba wa walimu, uchache wa vifaa vya kufundishia pamoja na malimbikizo ya madeni ya mishahara ya walimu .Hivyo ameiagiza  wizara ya elimu kuhakikisha wanawalipa  madeni yote  wanayodai  walimu  kabla ya kufikia mwaka 2019 kwani kuendeleza deni hilo litapunguza ari ya ufundishaji kwa walimu na kupelekea sekta ya elimu kushuka kutokana na maslahi madogo ya walimu.
Hata hivyo  Rais Shein amesema ameridhishwa na matokeo yaliyopatikana katika mitihani ya taifa  kwa elimu ya msingi na sekondari na kuitaka wizara ya elimu  kukaa pamoja na shule zote za Zanzibar zile  zilizofanya vibaya katika mitihani ya taifa ili kuweza kujua  sababu  zilizopelekea kufeli kwao kwenye mitihani hiyo.
Aidha amesema serikali itaendelea kujali na kuthamini michango ya walimu  yanayotoka katika taifa  kwa kujali maslahi yao.
 Akisoma risala ya walimu Katibu Mkuu wa chama cha walimu Zanzibar  Mussa Omar Tafurwa   amesema miongoni mwa matatizo yanayowakabili ni tatizo la uhaba wa walimu kwa shule za Pemba, mikoa ya Kaskazini  na Kusini  kwa Unguja.
Tafurwa ameiyomba serikali  kufanya uwekezaji wa  rasilimali   fedha ya kutosha ili kuweza kuajiri walimu ,kununulia vifaa vya kufundishia pamoja na  kulipa madeni ya walimu wanayodai kwani pia baadhi yao wamesha staafu na wengine wamekwishafariki.
Amesema pia licha ya matatizo hayo pia  walimu wanakabiliwa na mazingira magumu ya kufundishia ambapo hupelekea kuumwa na kushindwa kufanya kazi vizuri  hivyo wameiyomba serikali  kuwaanzishia bima ya afya  kwani wanashindwa mukumu gharama za matibabu  kwani fedha wanayoipata  bado haikidhi haja.

No comments