WAZIRI MWIGULU NCHEMBA APONGEZA JUHUDI ZA BODABODA ARUSHA NA KUWAUNGA MKONO KWA MILIONI 10
Na Paschal D.Lucas
Waziri wa mambo ya ndani Mh.Mwigulu Nchemba amepongeza juhudi na hatua ya umoja wa bodaboda jiji la Arusha(UBOJA) kwa kushirikiana na mkuu wa
Mkoa huo Mrisho Gambo kwa hatua kubwa ya kuimarisha umoja wa waendesha bodaboda
mkoani humo.
Akitoa pongezi hizo mbele ya mkuu wa mkoa, viongozi
wandamizi wa mkoa na umoja wa waendesha bodaboda wa Arusha kwenye kikao cha kuwakabidhi
vijana bodaboda kilichofanyika leo Machi 3,2018 katika ukumbi wa Mount Meru
Hotel jijini Arusha.
Naye Mkuu wa kitengo cha usalama barabarani wa mkoa
(RTO) aliyefahamika kwa jina moja la Bw.Bukombe amesema kuwa waliohitimu
mafunzo hayo ni jumla ya vijana 250 kwa wiki iliyopita na wengine zaidi ya mia
moja(100) wanatarajia kumalizia mafunzo yao siku ya jumatatu.
Bw.Bukombe ameunga mkono wazo la Mkurugenzi wa mamlaka
ya mapato( TRA) mkoa kwa kuwataka kuingia darasani wapate mafunzo ili waweze
kupata vyeti na leseni kwa njia sahihi.
Ameongeza kuwa bodaboda wanatakiwa kuvaa kofia ngumu na
kuwa wasafi kwa abiria wao na waachane na suala la ubebaji wa mishikaki na
kuheshimu alama za barabarani ikiwemo sehemu za wavuka miguu.
Mwenyekiti wa
umoja wa bodaboda jiji la Arusha(UBOJA) Bw.Maulid Makongolo mezitaja changamoto
wanazozipata wakati wa uendeshaji wa bodaboda jijini humo wakati akisoma risala
mbele ya Waziri Lazeck Nchemba kuwa ni pamoja na ulemavu na vifo kwa sababu ya
ajali, kutekwa na kunyang’anywa pikipiki na kupigwa,upinzani wa kisiasa, baadhi
ya viongozi kutotambua wanapohitaji msaada, na baadhi yao kutokuwa waaminifu
katika marejesho.
Alitaja pia malengo yao ni pamoja na kujua idadi halisi
ya waendesha pikipiki,kufungua miradi ya umoja,mfuko wa kusaidiana na kushiriki
shughuli za kijamii.
Baada ya mwenyekiti wa Umoja wa bodaboda jiji la Arusha
kusoma risala mbele ya waziri wa mambo ya ndani Mh.Mwigulu Nchemba Mkuu wa
wilaya ya Arusha Bw.Gabriel Ndakaro
alisema pikipiki zilizotolewa kwa waendeshaji hazikuwa na riba wala dhamana na sababu ya kutoa pikipiki hizo
ni kwa sababu ya wazi kabisa kuwa waendesha bodaboda ni watu wanyonge hivyo
wasingeweza kupata mkopo benki na baadhi ya wanasiasa kuwataka wasipaki na waondoke
maeneo ya benki na wasiingie mjini kabisa.
Lakini kupitia juhudi za viongozi walipambana na suala
hilo na halikuweza kutokea.Amewataka waweke utaratibu wa kuhakikisha bodaboda
wote waliosajiliwa kwenye umoja huo kutii na kufuata taratibu zote za sheria
ili kuimarisha umoja wao na kuleta ushikamano baina ya serikali na waendesha
bodaboda.
Akimkaribisha Mh.Mwigulu Nchemba Mkuu wa mkoa wa Arusha
Bw.Mrisho Gambo amemshukuru Mh.Waziri Mwigulu Nchemba kwa kukubali kushiriki
zoezi hilo na kuwashukuru watendaji wa ngazi zote kuanzia mkuu wa wilaya,
watendaji na maafisa tarafa kwa kusimamimia zoezi la ukusanyaji wa pesa
kufanikisha zoezi hilo na kuwataka watendaji kwenda kushiriki kutatua kero za
wananchi kama walivyoagizwa na serikali ya awamu ya tano.
Bw.Mrisho Gambo amewataka wananchi wa Arusha kuwa hakuna
suala la maandamano tena mkoani humo kwa sasa kama ilivyokuwa imezoeleka zamani
kwa viongozi wa vyama pinzani kuwatumia bodaboda kuanzisha maandamano hayo.
Ameongezea kuwa si kwa sasa kwani sasa hivi ni muda wa
kazi kutatua changamoto na kero za
wananchi nakuleta maendeleo na itabaki kuwa ni historian a kuwahakikishia kuwa
wamejipanga vizuri.
“Nataka niwahakikishie kwamba sisi tumejipanga vizuri, mtu yeyote kwa sababu
yeyote ambaye atatumwa kuja kupima kina cha maji tutamsaidia kuzama” Alisema
Alisisitiza suala la siasa kuwa tunataka siasa yenye
kuleta maendeleo na sio kubomoa kama ilivyokuwa imepangwa kwa bodaboda
kutoingia mjini bali waishie nje ya mji.
Bw.Mrisho Gambo alielezea pia suala la maendeleo ya mkoa
kuwa mpaka sasa wameanzisha ujenzi wa vituo vya afya katika kata mbalimbali na
Mh Rais Magufuli ametoa zaidi ya shilingi milioni 400 kwa ajili ya maendeleo ya
Mkoa wab Arusha.
Akijibu risala Mh.Lameck Nchemba amewataka vijana
kujiepusha na makundi mabaya yanayoleta uvunjifu wa amani nchini huku akiwataka
waepukane na ajali kwa kuzingatia taratibu za uendeshaji wa bodaboda kwa
kufuata alama zilizoko barabarani na kuhakikisha kuwa kila mwendesha bodaboda
awe na kofia ngumu mbili za kuendeshea pikipipiki kwa maana ya dereva na
abiria.
Mh. Mwigulu Nchemba amewashukuru watendaji na viongozi
wa ngazi zote za kijiji,kata, wilaya mpaka mkoa kwa juhudi zao za kuleta
maendeleo hususani kwa suala la ajira kwa vijana kwa kuwaunganisha na
kuwasaidia vijana kujiajiri kupitia kazi ya uendeshaji wa pikipiki(Bodaboda)
kwa kushirikiana na mkuu wa mkoa ambaye ni alama ya uaminifu na utendaji kazi
kwa ngazi ya mkoa.
“Serikali ya awamu ya tano chini ya Mh.Rais wa Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania Dk.John Pombe Magufuli imetuamini vijana kwa sababu ya
utendaji na uwajibikaji wetu kwa taifa, hivyo kupitia muunganiko huu na
ushirikiano huu wa viongozi wa ngazi zote na mkuu wa mkoa unatufanya tuzidi
kuonekana na kuaminika kwa taifa kuwa vijana tunaweza kiuntendaji” Alisema
Mh.Mwigulu Nchemba amewataka wamiliki na waendeshaji wa
bodaboda kufuata taratitu zote za umiliki wa pikipiki kwa kuhakikisha kuwa
pikipiki inakuwa na kofia mbili kwa dereva na abiria,leseni na kadi ya pikipiki
ndipo ihesabike kuwa imekamilika na kuondokana na ukamataji usio na heshima na
kuleta umoja ulio imara.
Mh.Mwigulu Nchemba amelitaka na kulikumbusha Jeshi la
Polisi nchini kuwa pikipiki ambazo zina makosa madogomadogo zilizoko vituoni
zirudishwa kwa wenye nazo
wakazirekebishe kuepukana kuwa chuma chakavu, lakini kwa pikipiki zenye
makosa yanayohitaji upelelezi na ushahidi ziendelee kubaki kwenye vituo vya
Polisi.
Ameongezea pia kuwa kila dereva boda boda ahakikishe
anavaa kofia na abiria wake.
“Kila pikipiki iwe na kofia mbili moja ya dereva na
nyingine ya abiria,kama abiria hatavaa ni kosa la abiria na sio mwendeshaji, na
kama pikipiki ina kofia moja tu ya dereva ni kosa la mwenye bodaboda hivyo
faini italipwa na aliyetenda kosa hilo” Alisema
Mh.Mwigulu Nchemba ameridhia ombi la mkuu wa mkoa la
kuwapa miezi mitatu waendesha bodaboda bila kukamata na kuongezea kuwa kuna
utaratibu wanaratibu pawepo na usawa
baina ya faini ya pikipiki na gari zingine kama costa nasio uliopo sasa
hivi.
Amemalizia kwa kupongeza mkuu wa mkoa kwa kufanya mpango
mkakati wa kuwafanikisha bodaboda
kufikia hatua hiyo na kuwaunga kwa mchango wa shilingi milioni kumi
(10,000,000) ili kuongeza jitihada za kuwapa vijana pikipiki zingine ili
wajikwamue kimaisha.
Umoja wa bodaboda jiji la Arusha (UBOJA) ulianzishwa
rasmi mwezi Disemba 2016 ukiwa na wanachama 200 mpaka sasa wako jumla ya
wanachama 500.
No comments