Header Ads

Wito wa usaili kwa wizara mbalimbali Pemba

Tume ya Utumishi Serikalini inawatangazia wale wote walioomba nafasi za kazi katika Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji, Wizara ya Afya, Kamisheni ya Wakfu na Mali ya Amana na Wizara ya Fedha na Mipango kwa nafasi za Pemba wanatakiwa kufika kwenye usaili kwa mujibu wa taasisi aliyoomba kwa utaratibu ufuatao:-
MCHANGANUO WA USAILI – PEMBA
1. WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI – PEMBA – Skuli ya Fidel – Castro Pemba saa 2:00 asubuhi
16/09/2017 • Walimu wa Ceti
17/09/2017 • Walimu Wa Diploma ya Msingi
18/09/2017 • Walimu Wa Digirii
2. WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI – PEMBA
a. 19/09/2017 – Skuli ya Fidel – Castro Pemba saa 2:00 asubuhi
• Ulinzi,
• Karani Masjala,
• Muhudumu,
• Karani Mapato,
• Afisa Utumishi na
• Dereva
b. 20/09/2017 – Skuli ya Fidel – Castro Pemba saa 2:00 asubuhi
• Waziba Mipira,
• Mkaguzi wa Magari,
• Fundi Mchundo,
• Fundi Mwashi,
• Fundi Umeme na
• Mfunga Maji
3. WIZARA YA AFYA – PEMBA tarehe 21/09/2017 Wizara ya Afya – Wete Pemba (Hospitali ya Wete) saa 2:00 asubuhi
• Afisa Tabibu Daraja la III
• Muuguzi wa Afya ya Akili
• Fundi Sanifu Madawa
• Afisa Afya Mazingira
4. KAMISHENI YA WAKFU NA MALI YA AMANA tarehe 22/09/2017 Kamisheni ya Wakfu – Pemba saa 2:00 asubuhi
• Afisa Uhusiano Mambo ya Kiislamu Msaidizi
5. WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO – PEMBA tarehe 22/09/2017 Wizara ya Fedha na Mipango – Pemba saa 2:00 asubuhi
• Katibu Muhtasi
Na Paschal D.Lucas

No comments